Aliyekuwa mshambuliaji hatari wa timu ya Yanga Mrisho Ngasa, amenunuliwa na timu ya Azam FC ambayo pia inashiriki ligi Kuu nchini kwa dau la milioni 58, mwaka huu timu hiyo imekamata nafasi ya tatu katika ligi hiyo , Ngasa anaweza kuwa mchezaji ghali zaidi kama hakutatokea mchezaji mwingine kununuliwa kwa dau kubwa kama hilo hapa Tanzania.
Hapo awali aliripotiwa kufukuziwa na timu ya jeshi la Rwanda APR lakini hatimaye kitendawili kimeteguka sasa mchezaji huyo ni mali ya Azam FC.
0 comments