Latest News

Jipangusee!! RRaaaaa!!


Lil - Kim, Bracket na ‘Aladji’ Leaders hapatoshi kesho

Baada ya shoo za mikoani, sasa ni zamu ya jiji kubwa kuliko yote, Dar ambapo Fiesta 2010 ‘Jipanguse Rrararaaaa’, itapoteza vilivyo ndani ya Viwanja vya Leaders Kinondoni kesho ikipambwa na wanamuziki wa kimataifa, Kimberly Denis Jones ‘Lil Kim’ kutoka Marekani, Bracket na Ramatulaye ‘Aladji’ kutoka Nigeria.

Stori kutoka kwa waratibu wa event hiyo, Prime Time Promotions zinaweka kweupe kwamba watanzania, kwa mara ya kwanza watapata nafasi ya kuwashuhudia wasanii hao waki-perform live kwenye jukwaa moja.

Taarifa hizo zinaeleza kwamba, hakuna mpenda burudani atakayekuwa na muda wa kukaa chini kwani burudani itakuwa ni non-stop mpaka kucheee!

Kuhusu viingilio ni buku kumi (10,000/) tu kabla ya event kuanza na buku kumi na tano (15,000) mlangoni.

Wasanii kibao Bongo nao watapata nafasi ya kuonesha shoo za ukweli. Baadhi ya wasanii hao ni pamoja na Mwasiti, Dully Sykes, Barnabas, Linah, Fid Q wengine wengi.

Source by Mrisho
Tags:

About author

Curabitur at est vel odio aliquam fermentum in vel tortor. Aliquam eget laoreet metus. Quisque auctor dolor fermentum nisi imperdiet vel placerat purus convallis.

0 comments

Leave a Reply